Best 741 quotes of Enock Maregesi on MyQuotes

Enock Maregesi

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Bila maskini tajiri hana maana!

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Abra maana yake ni fursa. Kwa hiyo, geuza matatizo yako kuwa fursa. Lakini, utageuzaje matatizo yako kuwa fursa? Kugeuza matatizo yako kuwa fursa, amini kama unaweza, usitumie muda mwingi kufikiria tatizo, tumia muda mwingi kufikiria fursa. Ukipata tatizo usikate tamaa. Badala yake, geuza tatizo hilo kuwa faida.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Accepting Jesus as your Lord and Savior is courage.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Acha alama katika dunia baada ya kuondoka.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Adam Kuambiana umerudi nyumbani ulikotoka, ukiongozwa na imani na mwanga wa wale uliowapenda na kuwapoteza. Hatuwezi kukumbuka kwamba umetutoka bila kukumbuka kwamba uliishi, na kwamba maisha yako yalitupa kumbukumbu nzuri tusizoweza kuzisahau haraka. Jumanne, siku ya kuuaga mwili uliokuwa ukitumiwa na wewe, wengine watasema Kwa heri lakini mimi nitasema Asante! Asante kwa sababu ya kipaji chako. Asante kwa sababu ya kujitahidi kwa kadiri ya uwezo wako wote, kutoa sauti kwa wale wote waliokuwa hawawezi kusikika. Asante kwa sababu ya kuacha dunia katika hali nzuri kuliko ulivyoikuta wakati ukiingia, na Asante kwa sababu ya maisha yako. Tukiendelea kuomboleza kifo cha Adam Kuambiana hapa duniani, wengine wanasherehekea kukutana naye huko mbinguni. Mchungaji wa uhai wa wote Mungu wa mbinguni ailaze roho yake mahali pema peponi: Yeye ni mwandishi wa hadithi ya maisha yetu na ndiye aliyeandika ukurasa wa mwisho wa hadithi ya Adam.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Adamu na Hawa walipotenda dhambi waligundua kuwa kumbe walikuwa na miili, walipogundua kuwa walikuwa uchi, kisha Mungu akawalaani. Miili yao ikakosa thamani mbele ya Mungu, sisi wote tukalaaniwa pamoja nao. Kwa Mungu hii miili haina thamani hata kidogo. Chenye thamani ni roho.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Adamu ndiye mtu wa kwanza kumjua Mungu.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Addiction isn't about using drugs. It's about what the drug does to your life.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Adui wa msalaba ni yule anayeipenda dunia badala ya Mungu, na rafiki wa msalaba ni yule anayempenda Mungu badala ya dunia.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Afrika imekaliwa na mizimu. Wazungu hawataweza kumaliza mali ya Afrika. Mali ya Afrika ni ya Waafrika wenyewe. Itamalizwa na sisi wenyewe.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Afrika isomeshe watu wake, na itumie vizuri mapato yanayotokana na mauzo ya rasilimali zake kwa faida ya jumla ya wananchi wa nchi zake, kusudi baadaye wawe wataalamu wa rasilimali za nchi zao wenyewe, kuepukana na utumwa wa rasilimali. Rasilimali za Afrika zina miiko na masharti yake.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Afrika si maskini! Uongozi wake ndiyo maskini.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Aidha, tunaweza kupata inkishafi kutokana na asili ya miili yetu, matukio fulani ya wakati ujao yana asili yake katika ndoto za binadamu. Ndoto hizo au maono hayo ni ishara ya kile kinachokuja mbele katika maisha ya mtu; kama vile afya, ugonjwa au hatari. Ukiota kuhusu moto, hiyo ni ishara ya hasira – unatakiwa kuwa na hekima; ukiota kuhusu mimba na unajifungua, hiyo ni ishara ya kuwa katika mchakato wa kutengeneza wazo jipya – unatakiwa kushukuru; ukiota unaruka angani, hiyo ni ishara ya tumaini – unatakiwa kushukuru; ukiota kuhusu maji au kiowevu kingine chochote kile, hiyo ni ishara ya siri na wakati mwingine ni ishara ya kuwa na matatizo ya kiafya kama utaota kuhusu maji machafu – unatakiwa kuwa msiri na msafi; ukiota kuhusu ardhi, hiyo ni ishara ya huzuni – unatakiwa kuomba; na ukiota kuhusu Yesu, hiyo ni ishara ya mafanikio – unatakiwa kushukuru.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Ajali haina mkanda. Punguza mwendo wa gari lako.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    A.K.A kirefu chake ni 'Also Known As'. K.K.K kirefu chake ni 'Kadhalika Kikijulikana Kama'. K.N.K kirefu chake ni 'Kadhalika Nikijulikana Kama'. K.A.K kirefu chake ni 'Kadhalika Akijulikana Kama'. Kadhalika, unaweza kusema P.K.K (Pia Kikijulikana Kama), P.N.K (Pia Nikijulikana Kama) au P.A.K (Pia Akijulikana Kama).Tujifunze kuupenda utamaduni wetu, ili vizazi vijavyo visisumbuke.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Akili yako isipokuwa timamu, familia itakushinda. Familia ikikushinda utalaumiwa na Mwenyezi Mungu.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Akili ya mipango ni bora kuliko akili ya darasani.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Akili yangu itakaponipeleka kwa mgonjwa hospitalini halafu sekunde hiyohiyo jicho langu likacheza au kiungo changu chochote cha mwili kikauma na kuacha ghafla ‘bila’ sababu yoyote, najua kile ninachokifikiria kuhusu mgonjwa huyo ama kitatokea au hakitatokea. Nikifikiria amepona, halafu ghafla kichwa kikaniuma na kuacha, kitakuwa kinyume chake. Yaani, hatapona. Nikifikiria amekufa, halafu ghafla kichwa au kiungo kingine chochote kikaniuma na kuacha, kitakuwa kinyume chake pia. Yaani, hatakufa. Hivyo, nikifikiria amepona, nikifikiria amekufa, na kichwa kikaniuma na kuacha, sekunde hiyohiyo natakiwa kumwombea mgonjwa huyo. Kama ni kupona, apone kama Mungu alivyokusudia; na kama ni kufa, afe kama Mungu alivyokusudia. Si kama Shetani alivyokusudia.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Akili ya peke yako haina maana. 2 + 2 = 5.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Amani ya moyo ndicho kipimo cha mafanikio yetu.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Amani ya nafsi ni zaidi ya amani ya kisiasa. Amani ya kisiasa itaweza kupatikana endapo watu watakuwa na amani ndani ya mioyo yao. Watu wakiithamini amani na kuielewa watayafurahia maisha yao, na mataifa yakiithamini amani na kuielewa yatastawi. Vita hutengenezwa ndani ya mioyo ya watu. Ukiitafuta amani ndani ya moyo wako, taifa halitasimama kupigana na taifa, amani itaweza kupatikana.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Amka, fumbua macho, uujue ukweli.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Anayejiua ameua na ameuwawa.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Anayesema fulani ni mwanachama wa chama cha siri cha kusaidiana cha wajenzi huru ana hakika? Haya mambo ni siri. Amejuaje? Kumbuka, usiamini, jua!

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    An Indian child is brought up in England, and he will speak both English and Hindi very well. English in school and Hindi at home. But here it’s English both in schools and at home. Why can’t you speak Swahili with your child at home? If this continues we will turn into an English speaking country.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Anza. Mungu mwenyewe atakuonesha njia.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Asiyefundishwa na wazazi wake atafundishwa na dunia kwa kudharaulika.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Askari wa Kirumi alimchoma Yesu mkuki ili andiko litimie. Askari huyo ambaye Biblia haikumtaja jina kwa sababu zilizoko nje ya uwezo wetu, alivyoona kweli amepona na ameona alishuhudia, na ushuhuda wake ulitoka moyoni, ili nasi tupate kusadiki. Wauaji wa Kirumi walipoona kwamba wale wezi waliosulubiwa pamoja na Yesu walikuwa bado hawajakata roho, waliwavunja miguu ili washindwe kupumua na hivyo kuharakisha kifo chao. Kwa upande wa Yesu, waliona alishapoteza fahamu na labda alishafariki. Kuthibitisha hilo askari wa Kirumi alirusha mkuki, nao ukatoboa utando unaozunguka moyo wa Yesu na mapafu ya Yesu, na damu na maji kutoka. Lakini yote hayo yalishatabiriwa miaka mingi kabla ya Yesu: ‘Hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa’ na ‘Nao watamtazama yeye ambaye walimchoma’.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    ATP hutumika katika kipindi ambapo mtu anakuwa amekata tamaa kabisa katika jambo lolote analolifanya, na yeyote anayetumia ATP ana uwezo mkubwa wa kufanikiwa katika maisha yake. Hivyo, usikate tamaa, jitahidi kwa kadiri ya uwezo wako WOTE.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    ATP inaweza kukusaidia kupata akili na nguvu ya kufanya jambo ambalo katika hali ya kawaida lisingewezekana. Wakati mwingine unaweza kufanya jambo hata wewe mwenyewe ukashangaa umelifanyaje. Unaweza kwa mfano kufukuzwa na mnyama mkali ukapenya mahali ambapo, katika hali ya kawaida usingepenya. Sasa usishangae tena. Kilichofanya upenye ni ATP.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Baada ya Adam na Hawa kutenda dhambi katika bustani ya Edeni, kila mtu anayezaliwa anazaliwa katika dhambi. Kwa hiyo dhambi hutokana na maisha, na maisha hutokana na dhambi.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Baada ya kuomba, tendo ambalo unapaswa kulifanya kila siku, endelea kuomba kwa kushukuru na kumsifu Mungu hadi jibu lako litakapofika. Kwani, ulivyoomba mara ya kwanza Mungu alikusikia na alikujibu papo hapo!

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Badilisha tabia. Badilisha mazingira ya maisha yako. Haijalishi una umri kiasi gani au wewe ni mwanamke au mwanamume, bado hujachelewa kubadili maisha yako kutoka duni kuwa bora – kuwa na amani, furaha na kuridhika. Kama desturi yako ni kuamka saa 12:00 asubuhi kila siku ili ufike kazini saa 2:00 asubuhi ambao ni muda wa serikali wa kuanza kazi, amka saa 11:30 asubuhi ili ufike kazini saa 1:30 asubuhi – nusu saa kabla ya kuanza kazi. Kama unafanya kazi ya taaluma uliyosomea lakini maisha hayaendi, fikiria kubadili mwelekeo wa maisha ikiwemo taaluma kufikia malengo uliyojiwekea.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Baraka inapotoka kwa Mungu lengo lake ni kukufanya umpende Mungu kupitia wenzako.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Bara la Afrika ni tajiri kwa rasilimali kuliko mabara yote duniani. Lakini ni maskini kuliko mabara yote. Cha muhimu si kuwa na rasilimali ardhini. Cha muhimu ni kuwa na rasilimali sokoni.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    BASATA (Baraza la Sanaa la Taifa) hawataweza kukutambua kwa sababu hujajisajili kwao, na kushirikiana na msanii ambaye hajajisajili BASATA ni kinyume cha sheria.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Behave professionally and let any bad feelings out of life!

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Beroendet är inte om att använda droger. Det handlar om vad läkemedlet gör att ditt liv.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Bethlehemu iliteuliwa na Mungu kuwa mahali pa kuzaliwa Mfalme. Kwa sababu ya Bethlehemu, dhambi zetu zote zilisamehewa. Wakristo wengi wakipata pesa wanakwenda Dubai, China, Marekani, Uingereza, na mahali pengine kutalii. Lakini hawaendi Bethlehemu.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Biblia inatuagiza tuwaheshimu wazazi wetu ili siku zetu zipate kuwa nyingi hapa duniani. Mzazi wako akikutuma kuiba mheshimu kwa kukataa.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Bibi Martha Maregesi aliishi maisha mazuri sana hapa duniani. Alibarikiwa na Mungu. Aliishi miaka 84 – siku 30660 badala ya siku 25550 tulizopangiwa na Mungu. Katika uhai wake wote, kwa wale wote aliowalea, hakuna mtoto wake hata mmoja aliyefariki kabla yake. Hakuna mjukuu wake hata mmoja aliyefariki kabla yake. Hakuna kitukuu chake hata kimoja kilichofariki kabla yake. Bibi yangu ametimiza mwaka mmoja kamili leo hii, tangu amefariki dunia Novemba 4 mwaka 2014 mjini Musoma. Tunamkumbuka leo akiwa amefariki kama tulivyomkumbuka jana akiwa hai. Nguvu ya sala zetu imfanye Mwenyezi Mungu aendelee kumsamehe dhambi zake zote, na amweke mahali anapostahili, Amina.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Biblia inatuambia kuwa tuombe bila kukoma. Lakini tutaombaje bila kukoma? Njia mojawapo ya kufanya hivyo ni kutumia ‘maombi ya pumzi’ kila siku kama ambavyo Wakristo wengi wamekuwa wakifanya kwa karne nyingi. Unachagua sentensi fupi au maneno rahisi kuhusu Yesu unayoweza kuyasema na kuyarudia kimoyomoyo kila siku katika kila pumzi inayoingia na kutoka ndani ya mapafu yako! Kwa mfano: “Asante Yesu.” “U pamoja nami.” “Nataka kukujua.” “Napokea neema yako.” “Nakutegemea wewe.” “Mimi ni wako.” “Nisaidie nikuamini.” “U Mungu wangu.” “Naishi kwa ajili yako.” “Nisamehe dhambi zangu zote.” Fundisha akili yako kumkumbuka Mungu kila wakati.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Biblia ni kiwanda cha imani.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Biblia pamoja na historia vinatwambia kuwa mitume kumi na wawili wa Yesu Kristo waliamua kufa kinyama kama mfalme wao alivyokufa, kwa sababu walikataa kukana imani yao juu ya Yesu Kristo. Mathayo alikufa kwa ajili ya Ukristo nchini Ethiopia kwa jeraha lililotokana na kisu kikali, Marko akavutwa na farasi katika mitaa ya Alexandria nchini Misri mpaka akafa, kwa sababu alikataa kukana jina la Yesu Kristo. Luka alinyongwa nchini Ugiriki kwa sababu ya kuhubiri Injili ya Yesu Kristo katika nchi ambapo watu hawakumtambua Yesu. Yohana alichemshwa katika pipa la mafuta ya moto katika kipindi cha mateso makubwa ya Wakristo nchini Roma, lakini kimiujiza akaponea chupuchupu, kabla ya kufungwa katika gereza la kisiwa cha Patmo (Ugiriki) ambapo ndipo alipoandika kitabu cha Ufunuo. Mtume Yohana baadaye aliachiwa huru na kurudi Uturuki, ambapo alimtumikia Bwana kama Askofu wa Edessa. Alikufa kwa uzee, akiwa mtume pekee aliyekufa kwa amani. Petro alisulubiwa kichwa chini miguu juu katika msalaba wa umbo la X kulingana na desturi za kikanisa za kipindi hicho, kwa sababu aliwaambia maadui zake ya kuwa alijisikia vibaya kufa kama alivyokufa mfalme wake Yesu Kristo. Yakobo ndugu yake na Yesu (Yakobo Mkubwa), kiongozi wa kanisa mjini Yerusalemu, alirushwa kutoka juu ya mnara wa kusini-mashariki wa hekalu aliloliongoza la Hekalu Takatifu (zaidi ya futi mia moja kwenda chini) na baadaye kupigwa kwa virungu mpaka akafa, alipokataa kukana imani yake juu ya Yesu Kristo. Yakobo mwana wa Zebedayo (Yakobo Mdogo) alikuwa mvuvi kabla Yesu Kristo hajamwita kuwa mchungaji wa Injili yake. Kama kiongozi wa kanisa hatimaye, Yakobo aliuwawa kwa kukatwa kichwa mjini Yerusalemu. Afisa wa Kirumi aliyemlinda Yakobo alishangaa sana jinsi Yakobo alivyolinda imani yake siku kesi yake iliposomwa. Baadaye afisa huyo alimsogelea Yakobo katika eneo la mauti. Nafsi yake ilipomsuta, alijitoa hatiani mbele ya hakimu kwa kumkubali Yesu Kristo kama kiongozi wa maisha yake; halafu akapiga magoti pembeni kwa Yakobo, ili na yeye akatwe kichwa kama mfuasi wa Yesu Kristo. Bartholomayo, ambaye pia alijulikana kama Nathanali, alikuwa mmisionari huko Asia. Alimshuhudia Yesu mfalme wa wafalme katika Uturuki ya leo. Bartholomayo aliteswa kwa sababu ya mahubiri yake huko Armenia, ambako inasemekana aliuwawa kwa kuchapwa bakora mbele ya halaiki ya watu iliyomdhihaki. Andrea alisulubiwa katika msalaba wa X huko Patras nchini Ugiriki. Baada ya kuchapwa bakora kinyama na walinzi saba, alifungwa mwili mzima kwenye msalaba ili ateseke zaidi. Wafuasi wake waliokuwepo katika eneo la tukio waliripoti ya kuwa, alipokuwa akipelekwa msalabani, Andrea aliusalimia msalaba huo kwa maneno yafuatayo: "Nimekuwa nikitamani sana na nimekuwa nikiitegemea sana saa hii ya furaha. Msalaba uliwekwa wakfu na Mwenyezi Mungu baada ya mwili wa Yesu Kristo kuning’inizwa juu yake." Aliendelea kuwahubiria maadui zake kwa siku mbili zaidi, akiwa msalabani, mpaka akaishiwa na nguvu na kuaga dunia. Tomaso alichomwa mkuki nchini India katika mojawapo ya safari zake za kimisionari akiwa na lengo la kuanzisha kanisa la Yesu Kristo katika bara la India. Mathiya alichaguliwa na mitume kuchukua nafasi ya Yuda Iskarioti, baada ya kifo cha Yuda katika dimbwi la damu nchini India. Taarifa kuhusiana na maisha na kifo cha Mathiya zinachanganya na hazijulikani sawasawa. Lakini ipo imani kwamba Mathiya alipigwa mawe na Wayahudi huko Yerusalemu, kisha akauwawa kwa kukatwa kichwa. Yuda Tadei, ndugu yake na Yesu, aliuwawa kwa mishale alipokataa kukana imani yake juu ya Yesu Kristo. Mitume walikuwa na imani kubwa kwa sababu walishuhudia ufufuo wa Yesu Kristo, na miujiza mingine. Biblia ni kiwanda cha imani. Tunapaswa kuiamini Biblia kama mitume walivyomwamini Yesu Kristo, kwa sababu Biblia iliandikwa na mitume.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Bila dhambi hakuna msamaha.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Bila kiburi hutamshinda Shetani, lakini kiburi dhidi ya Shetani unakishinda kwa hekima.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Bila kujali dini ya mtu, bila kujali anaamini nini, kila mtu anatakiwa kujua kusudi la maisha yake.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Binti yako mwenye umri wa miaka kumi na nne kwa mfano, anaomba umnunulie gari kama ulivyofanya kwa kaka yake mwenye umri wa miaka kumi na nane. Mara ya kwanza unamwambia utamnunulia atakapofikisha umri wa miaka kumi na nane kama ulivyofanya kwa kaka yake. Lakini baada ya wiki moja binti yako anakuomba tena kitu kilekile, yaani gari. Utajisikiaje? Utakereka, sivyo? Jinsi utakavyokereka binti yako kukuomba kitu ambacho tayari ameshakuomba, ndivyo Mungu anavyokereka sisi kumwomba vitu ambavyo tayari tumeshamwomba. Ukiomba kitu kwa mara ya kwanza Mungu amekusikia, tayari ameshaandaa malaika wa kukuletea jibu. Unachotakiwa kufanya, baada ya kuomba, shukuru mpaka jibu lako litakapofika. Mungu huthamini zaidi maombi ya kushukuru kuliko maombi ya kuomba. Binti yako anachotakiwa kufanya baada ya kukuomba gari ni kukushukuru mpaka gari yake itakapofika, si kukuomba mpaka gari yake itakapofika.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Boresha maisha ya watu kwa kadiri utakavyoweza. Ukisaidia mtu 1 watahurumiwa watu 10. Ukisaidia watu 10 watahurumiwa watu 100. Ukisaidia watu 100 watahurumiwa watu 1000. Kila mmoja wetu akitambua wajibu wake katika jamii, Mungu atatuhurumia sisi wote. Maisha ya mtu mmoja yakiboreka, mmoja huyo ataboresha na ya wengine wengi. Hivyo, endelea kuogelea lakini usisahau kurudi nyuma katika jamii.

  • By Anonym
    Enock Maregesi

    Chukia kushindwa, zaidi ya unavyofurahia kushinda.